Font Size
Luka 9:18-21
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 9:18-21
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Petro Atambua Yesu ni Nani
(Mt 16:13-19; Mk 8:27-29)
18 Wakati mmoja Yesu alikuwa anaomba akiwa peke yake. Wafuasi wake walimwendea na aliwauliza, “Watu wanasema mimi ni nani?”
19 Wakajibu, “Baadhi ya watu wanasema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine wanasema wewe ni Eliya, lakini wengine wanasema wewe ni mmoja wa manabii wa zamani aliyefufuka.”
20 Kisha Yesu akawauliza wafuasi wake, “Na ninyi mnasema mimi ni nani?”
Petro akajibu, “Wewe ni Masihi kutoka kwa Mungu.”
21 Yesu akawatahadharisha wasimwambie mtu yeyote.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Copyright © 2017 by Bible League International